Saturday, 24 March 2012

ALINIPA KUMBI, ALEKUPA KITI



Ujapo kwasika, mtulivu uwe
Alipenda Rabuka, nilivyo niwe
Ikujiapo fanaka, adilika wewe
Alinipa kumbi, alekupa Kiti

Kazi niitendayo, yanikimu daima
Naipenda hiyo, iwapo ni rukwama
Yangu kazi hiyo, wewe ipe heshima
Alinipa kumbi, alekupa Kiti

Manani kanipa, hii yangu sura
We heshima nipa, niwapo chotara
Kama baya kanipa, nawe nzuri sura
Alinipa kumbi, alekupa Kiti

Nikaapo pale, paheshimu wewe
Kibadangu kile, chakuhusu ni we?
Shukuru Molale, kwa ulipo wewe
Alinipa kumbi, alekupa Kiti

Hata kama mie, sikupata elimu
Si penzi langu wee, kut’ona mwalimu
Tulivyo tukae, sote binadamu
Alinipa kumbi, alekupa kiti

Kafanya duniani, tufautiane
Lengole Manani, zoteni Karne
Sote duniani, tushirikiane
Alinipa kumbi, alekupa Kiti.

No comments:

Post a Comment